Obama Achanika Mdomo Baada ya Kupigwa 'Kipepsi'

Obama alikuwa akicheza mpira wa kikapu pamoja na ndugu na jamaa kwenye kambi ya jeshi la Marekani ya Fort McNair mjini Washington, wakati kwa bahati mbaya mcheza wa timu pinzani aliporusha kiwiko chake na kumtandika Obama mdomoni.

Msemaji wa ikulu ya Marekani alisema kuwa Obama alipasuka mdomo na alipatiwa matibabu na madaktari wa ikulu.

Hata hivyo taarifa ya ikulu ya Marekani haikusema ni nani ndiye aliyempasua Obama mdomo wake kwa kiwiko.

No comments:

Post a Comment